Habari zaidi zinasema kuwa, watu wawili wanaoaminiwa kuwa wanachama wa kundi la kigaidi na wakufurishaji la Daesh au ISIS ndio waliojiripua katikati ya Waislamu wakati wa Swala. Duru za hospitali zinasema kuwa, wengi wa majeruhi wako katika hali mbaya. Majengo yaliyo karibu na msikiti huo wa al-Balili yameharibiwa kabisa. Hadi tunakwenda hewani hakuna kundi lolote lilikuwa limedai kuhusika na mashambulizi hayo ya kinyama ingawa hujuma hiyo inafanana mno na mashambulizi ya huko nyuma ya Daesh au ISIS dhidi ya Mashia nchini Yemen. Tayari viongozi mbalimbali wa Kiislamu wamelaani hujuma hiyo kwenye msikiti na katika siku tukufu ya Idul-Adh’ha.