IQNA

Maafa ya Mina

Mfalme wa Saudia atoa mkono wa pole kwa Iran

7:19 - October 02, 2015
Habari ID: 3377239
Mfalme Salman wa Saudi Arabia ametoa mkono wa pole kwa serikali na watu wa Iran kufuatia vifo vya Wairani katika maafa yaliyojiri Mina karibu na Makka wakati wa ibada ya Hija hivi karibuni.

Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, gazeti la Saudi Arabia la Al Riyadh limeandika kuwa ujumbe huo wa rambi rambi umepokewa na Waziri wa Afya wa Iran Sayyid Hassan Hashimi alipokutana na mwenzake wa Saudi Arabia Khalid bin Abdulaziz Al-Falih mjini Jeddah. Katika kikao hicho mawaziri hao wawili walijadili maafa ya Mina na hali ya waliojeruhiwa waliolazwa katika hospitali za Saudia.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, Khalid bin Abdulaziz Al-Falih  aliwasilisha salamu za rambi rambi za mfalme wa Saudi Arbaia kwa serikali ya Iran na familia za waliopoteza maisha katika maafa ya mina na kusema ufalme huo uko tayari kushirikiana na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Gazeti hilo la Saudia limeandika kuwa waziri wa afya wa Iran amemshukuru mwenzake wa Saudia kwa kuandaa kikao hicho na ametaka  majeruhi wa Iran wapewe huduma zinazofaa za kitiba. Aidha pande mbili ziliafikiana kuhusu kuharakishwa kutambuliwa na kukabidhiwa Iran viwiliwili vya Mahujaji wote Wairani walipoteza maisha kwa ajili ya mazishi.../mh

3377002

Kishikizo: saudia iran mina maafa mfalme
captcha