Idara ya Usimamizi wa Harmain (Misikiti Miwili Mitakatifu ya Makka na Madina) umetangaza mipango muhimu ya Umrah wanaotembelea Msikiti Mkuu katika Ramadhani.
Ili kuhakikisha uzoefu mzuri kwa waumini wote, Tawaf katika eneo la chini la Kaaba itakuwa maalum kwa ajili ya wanaotekeleza ibada ya Umrah katika Mwezi huu.
Waumini wanaofika katika Msikiti Mtakatifu wa Makaa ambao hawafanyi Umrah wataweza kufikia sakafu ya juu ya Kaaba kwa ajili ya Tawaf wakati wa Ramadhani, eneo ambalo lina nafasi ya kutosha kwa kila mtu.
Uongozi pia umekamilisha uteuzi wa maimamu (viongozi wa swala) ambao wataongoza swala maalum ya Tarawehe na Tahajjud katika kipindi chote cha Ramadhani.
3487437