Ajali hiyo ilitokea katika barabara ya Aqaba Shaar inayounganisha mji wa Abha na mkoa wa Mahayil Asir.
Basi la abiria lilipoteza mwelekeo kufuatia kufeli breki na kugonga daraja na kupinduka na kuwaka moto. Wasafiri walikuwa wakielekea Makka kufanya Umra.
Vikosi vya Ulinzi wa Raia na Hilali Nyekundu ya Saudia pamoja na mamlaka za usalama walikimbilia eneo la tukio baada ya kupata taarifa kuhusu ajali hiyo na kuanza shughuli za uokoaji.
Mwendo wa trafiki ulitatizwa kando ya barabara kwa saa kadhaa kufuatia ajali hiyo. Miili ya waliopoteza Maisha na majeruhi imepelekwa katika hospitali kadhaa mkoani humo.
3482964